Friday, October 29, 2010

NAAM WAJUMBE!!!!!

habari zenu waungwana, ni matumaini yangu mpo gado kabisa na ikizingatiwa tarehe 31 tunaenda kufanya mabadiliko makubwa ya nchi yetu, naomba nitumie fursa hii kuwahimiza ndugu wajumbe kufanya kweli pasipo kuwa na hofu yoyote kuhakikisha kwamba kura yako moja inamchagua RAIS wa ukweli ambaye atajali maslahi ya nchi, wanachi na ya vijana pia au vp! so, stand up and go to vote!!!!

pia ndugu wajumbe harakati za kundi letu bado zinaendelea kama tulivyokubaliana kufanya biashara ya mavazi basi ni wajibu wetu kufanya utatifi wa kisayansi ili kwamba hili lengo letu litimie vizuri, unaombwa katika kikao kijacho uje na data za uhakika kuhusu hiyo business ili ikiwezekana mchakato uanze maramoja mara baada ya kumchagua RAIS makini.

kila la heri wajumbe katika uchaguzi huu nawaombea kwa Mungu awaongoze vema katika mpango mzima wa kuchagua viongozi wetu.